24.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Ofisa Tanesco mbaroni kwa kuomba rushwa ya ngono

FLORENCE SANAWA – MTWARA 

Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa mkoani Mtwara imemkamata ofisa Utumishi  wa Shirika la umeme Tanzania (Tanesco), Jumanne Songoro kwa tuhuma za kuomba rushwa ya ngono kwa mtumishi mwenzake ili ampangie majukumu mengine ya kazi Katika kitengo cha kudumu.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake leo Jumanne Julai 9, kamanda wa Takukuru mkoa wa mtwara Stephen Mafipa amesema afisa huyo amekamatwa baada ya kupata taarifa kutoka kwa mlalamikaji na baada ya uchunguzi waliweka mtego na kufanikiwa Kimkamata mtuhumiwa. 

Mafipa amesema katika mtego huo walifanikiwa kumkuta mlalamikaji akiwa na afisa huyo kwenye moja ya nyumba za wageni ambapo uchunguzi umebaini kuwa mtuhumiwa alianza kushawishi rushwa ya ngono tangu Desemba 2018 hadi juni 4 mwaka huu ambapo mlalamikaji aliwasilisha malalamiko hayo Takukuru kwa lengo la kupata msaada.

“Kwa majibu wa mlalamikaji mtuhumiwa alitaka rushwa hiyo kutoka kwa mtmishi mwenzake ili ampangie majukumu mengine ya kazi Katika kitengo cha kudumu kulingana na kiwango cha elimu baada ya kubadilishiwa majukumu ya awali kufuata maagizo kutoka makao makuu ya Tanesco,” amesema Mafipa.

Mtuhumiwa atafikishwa mahakamani na kufunguliwa mashtaka chini ya kifungu cha 25 cha sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa baada ya kukamilisha taratibu za kisheria. 

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles