WIKI iliyopita ilikuwa ngumu kwa msanii wa muziki nchini Marekani, Big Sean, baada ya nyumba yake kuvamiwa na watu wasiojulikana.
Wakati wa tukio hilo la uvamizi msanii huyo hakuwepo nchini Marekani ambapo watu hao walifanikiwa kuchukua vitu mbalimbali vikiwamo pamoja na cheni za dhahabu na kompyuta ambayo ilikuwa na nyimbo zake mpya.
Msanii huyo amesema baada ya kupiga hesabu ya vitu ambavyo vimepotea kutokana na wizi huo thamani yake imefikia zaidi ya milioni 300.
“Ninaamini tukio hili limefanywa na watu wangu wa karibu, inawezekana ikwa ni ndugu zangu wa karibu kwa kuwa wao ndio waliokuwa wanajua kwamba sipo nchini na familia yangu,” alisema Big Sean.