25.7 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

NYALANDU AITAKA KATIBA YA WARIOBA

Na NORA DAMIAN-DAR ES SALAAM

MBUNGE wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu (CCM), amesema anakusudia kuwasilisha muswada binafsi bungeni utakaoweka sharti la kurejewa mjadala wa Katiba Mpya.

Akizungumza na MTANZANIA jana, alisema muswada huo atauwasilisha katika kikao cha tisa cha Bunge kinachotarajiwa kuanza Novemba 7  mwaka huu mjini Dodoma.

Alisema Katiba ya nchi ni mkataba wa wananchi ambao utadumu kwa miaka mingi hivyo hautakiwi kufanywa kama dharura au kuogopwa bali unahitaji umakini.

“Mchakato ulianza ukatumia fedha nyingi na kuhusisha watu wengi lakini haukukamilika, na hapa katikati ulighubikwa na sintofahamu nyingi.

“Na kwa namna yoyote ile ili tuweze kuwa na Katiba bora itakayohusisha wadau wote kwa maana ya wananchi, viongozi wa vyama vya siasa na upande wa serikali itakuwa ni muhimu mchakato uanze kwa kuzingatia rasimu ya katiba kama ilivyowasilishwa na Tume ya Jaji Warioba,” alisema Nyalandu.

Alisema anatarajia kuwa wabunge wa chama chake na wabunge wa upinzani watamuunga mkono   hoja hiyo iweze kurudi upya na wadau wote wapate fursa ya kujadili ipatikane Katiba Mpya.

“Wabunge tuna nafasi yetu ya kujadili na kupeleka maoni ya binafsi na yale ya pamoja.

“Katiba imempa nafasi mbunge mmoja mmoja bila kujali ametoka chama gani, hivyo mimi naona ni hoja ambayo ni lazima ipate nafasi kama hoja nyingine na kufanyiwa kazi.

MATOKEO YA TWAWEZA

Wakati huohuo, Taasisi ya Twaweza jana ilitangaza matokeo ya utafiti ambayo yanaonyesha Watanzania wawili kati ya watatu wanahitaji Katiba Mpya.

Utafiti huo uliopewa jina la ‘Zege Imelala’ ulilenga kupata maoni ya wananchi kuhusu kukwama kwa mchakato wa kuunda Katiba Mpya.

Akitangaza matokeo hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa Twaweza, Aidan Eyakuze, alisema ulifanyika kati ya Juni hadi Julai mwaka huu na kuhusisha watu 1,745 kutoka maeneo mbalimbali ya Tanzania Bara.

“Asilimia 67 ya Watanzania wanasema ni muhimu kwa Tanzania kupata katiba mpya na nusu ya wananchi wanasema mchakato wa katiba uanze upya na tume mpya,” alisema Eyakuze.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles