25.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

NELLY ATUHUMIWA KUBAKA

OLYMPIA, WASHINGTON


NYOTA wa muziki wa hip hop nchini Marekani, Cornell Haynes ‘Nelly’, ameripotiwa kukamatwa na polisi kwa tuhuma za kubaka mwanamke kwenye gari yake.

Kwa mujibu wa mtandao wa TMZ, msanii huyo mwenye umri wa miaka 42, alikuwa kwenye basi lake kwenye ziara ya muziki huko Washington, hivyo msanii huyo alikuwa na mwanamke kwenye gari hiyo na hatimaye kumbaka saa 9 45 usiku.

Msanii huyo na wenzake walikuwa wanatarajia kufanya shoo kwenye tamasha mjini Ridgefield mwishoni mwa wiki iliyopita, lakini hadi sasa inadaiwa kuwa yupo chini ya ulinzi wa polisi, huku uchunguzi ukiendelea kufanyika.

Mwanasheria wa msanii huyo, Scott Rosenblum, aliweka wazi kuwa mteja wake amekuwa akituhumiwa mara kwa mara na mambo ya kutengenezwa, hivyo hakuna ukweli wowote juu ya tukio hilo.

 

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles