24.1 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

NCHI ZA AFRIKA KUINGIA AFRIKA KUSINI BILA VISA

Na Arodia Peter, Kigali

Rais wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa amesema kuanzia sasa Waafrika wataingia nchini humo bila kuhitajika kuwa na Visa.

Akizungumza katika mjadala wa kiuchumi uliousisha baadhi ya marais wa Afrika leo Jijini Kigali Rwanda, Ramaphosa amesema huu ni wakati wa Afrika kusonga mbele kwa kutumia fursa zinazoweza kupatikana.

“Kuanzia sasa watu wa Afrika wawe huru kuja kwetu, makubaliano haya yawe chachu ya kufungua milango kwetu sisi kama nchi huru na mawazo huru,” amesema Ramaphosa.

Aidha rais huyo mpya wa Afrika Kusini amempongeza Rais Paul Kagame wa Rwanda kwa kutilia mkazo ajenda hiyo ambayo alisema inaiweka Afrika katika histioria nyingine mpya.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles