26.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

NAPE AONGOZA WAOMBOLEZAJI KUMUAGA AMINA

Baadhi ya Waandishi wa Habari toka vyombo mbalimbali, wakiwa wamebeba jeneza lenye mwili wa aliyekuwa Mwandishi wa Habari za Michezo wa gazeti la Uhuru, Amina Athuman, baada ya kuwasili nyumbani kwao Kipunguni A jijini Dar es Salaam jana, kabla kusafi rishwa kwenda mkoani Tanga kwa maziko yanayotarajiwa kufanyika leo.
Baadhi ya Waandishi wa Habari toka vyombo mbalimbali, wakiwa wamebeba jeneza lenye mwili wa aliyekuwa Mwandishi wa Habari za Michezo wa gazeti la Uhuru, Amina Athuman, baada ya kuwasili nyumbani kwao Kipunguni A jijini Dar es Salaam jana, kabla kusafi rishwa kwenda mkoani Tanga kwa maziko yanayotarajiwa kufanyika leo.

NA JESSCA NANGAWE

WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye, jana aliongoza mamia ya waombolezaji katika kuuaga mwili wa aliyekuwa mwandishi wa habari za michezo na burudani, Amina Athuman, jijini Dar es Salaam.

Amina alikuwa mwandishi wa Kampuni ya Uhuru Publication wanaochapisha  magazeti ya Uhuru, Mzalendo na Burudani.

Mwili wa marehemu Amina, aliyefariki katika Hospitali ya Mnazi Mmoja iliyopo visiwani Zanzibar alipokwenda kuripoti mashindano ya Kombe la Mapinduzi  kutokana na matatizo ya uzazi, unatarajiwa kuzikwa leo nyumbani kwao Tanga.

Akizungumza baada ya mwili huo kuwasili, Nnauye alisema tasnia ya michezo imempoteza mmoja wa waandishi wachapakazi, aliyekuwa akifanya kazi zake kwa umakini mkubwa huku akiitaka familia yake kuwa na moyo wa subira kufuatia kifo hicho.

“Alikua ni moja ya waandishi wenye kujituma sana katika kazi yake, tulifahamu uwezo wake, kikubwa ni kumwombea makazi mema huko alipo, yeye ametangulia na sisi tupo nyuma yake, tunawapa pole wanafamilia kutokana na msiba huu mzito,” alisema Nnauye.

Marehemu Amina ameacha mume na mtoto mmoja wa kike, Yusra.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles