31.7 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

NAMELOK: MIMI SI MSAKA TONGE

|Eliya Mbonea, Arusha



Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi (NEC), kupitia Jumuiya ya Wazazi (UWT) Namelok Sokoine ameibuka na kudai kwamba yeye si mwanasiasa msaka tonge kama ilivyo kwa wasiasa wengine.

Kauli hiyo ameitoa mjini hapa baada ya kudaiwa kuhusika katika mpango wa kuandaa baadhi ya wana CCM waliovamia ofisi za chama hicho Wilaya ya Monduli wakipinga mpango wa kupendekeza jina la mwanachama mpya wa CCM, Julius Kalanga, aliyekuwa Mbunge wa Jimbo hilo kupitia Chadema.

Akizungumza na Mtanzania Digital, Sokoine aliyegombea ubunge kwenye uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 akichuana na Kalanga amesema, kwa kawaida yeye ni mwanasiasa na mtu asiyejificha hivyo kama angekuwa na nia ya kutaka kugombea kwenye uchaguzi mdogo hilo lisingekuwa tatizo kwake.

“Watu wasiogope vivuli vyao, mimi si mtu wa kujificha mwaka 2015 nilisimama kukipigania chama changu ingawa wengine walikimbia kusaka tonge, hivyo utaona kwa jinsi gani mimi si msaka tonge ni mwana CCM ninayekipenda na kukitahimini chama changu.

“Hao wanaodai kwamba wananchi waliofika Ofisi za CCM wilaya kuelezea kero zao kuhusu kanuni kuwa wanatoka kata za marafiki zangu naomba niwaambie hizo si kata za mtu ni kata zinazoongozwa na CCM na ndiyo zilizompa ushindi Rais John Magufuli mwaka 2015,” amesema.

Mwisho.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles