25.2 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

MWALIMU MKUU ADAIWA KUMUUA MWANAFUNZI KWA VIBOKO

NA FRANCIS  GODWIN- IRINGA

JESHI  la  Polisi  mkoani  Iringa linamshikilia Mwalimu  Mkuu  wa  Shule ya  Msingi, Ng’ingula, Wilaya ya Kilolo,  Robson Sanga (59),  kwa  tuhuma za  kumua mwanafunzi  wa  darasa la tano, Emmanuel Gavile (13) kwa kumchapa fimbo mapajani  kwa   kuchelewa shuleni.

Kamanda wa  Polisi wa  Mkoa wa Iringa,  Julius Mjengi, alisema  tukio  hilo  lilitokea Agosti 16, mwaka huu saa 3.00 asubuhi shuleni hapo baada ya mwanafunzi huyo kudaiwa kuchelewa kufika shuleni kwa muda ambao shule imeuweka.

Alisema  kutokana na adhabu hiyo, Gavile alilia kwa maumivu makali na kushindwa kujisomea hali iliyowafanya  wenzake    kumkimbiza katika zahanati ya  kijiji  hicho ambako hali  ilizidi  kuwa mbaya.

Baadaye alihamishiwa  Kituo cha  Afya  Usokomi wilayani humo.

“Agosti  26 mwaka huu mwanafunzi huyo alihamishiwa katika  Hospitali ya  Rufaa ya  Mkoa  wa Iringa akilalamikia  maumivu makali katika paja  la mguu wa  kulia kabla ya  kufariki dunia saa 3.00 asubuhi,” alisema Mjengi.

Kamanda   alisema     uchunguzi  wa daktari  umeonyesha  kuwa  kifo  cha mwanafunzi  huyo kilisababishwa na kupasuka  mfupa  wa paja la mguu  wa kulia na damu kuviria katika  mapafu yake.

Alisema kwa  muda  wote  huo  wazazi  hawakuweza  kuripoti polisi  ila  baada ya kifo cha mwanafunzi  huyo ndipo walipofika kituo cha polisi kutoa taarifa na jeshi hilo limemkamata  mwalimu huyo kwa uchunguzi.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles