24.1 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Mpango: serikali haijazuia ripoti ya IMF

Maregesi Paul, Dodoma

Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Phillip Mpango, amesema Serikali haijalizuia Shirika la Fedha Duniani (IMF) kuchapisha ripoti ya uchumi wa Tanzania isipokuwa kinachofanyika ni mazungumzo kati ya serikali ya Tanzania na shirika hilo kabla ripoti hiyo haijachapishwa.

Dk. Mpango ametoa taarifa hiyo bungeni leo Jumanne aprili 23, alipokuwa akitoa ufafanuzi wa maelezo ya Mbunge wa Tunduma, Frank Mwakajoka (Chadema), aliyesema Serikali imelizuia shirika hilo kutoa ripoti ya uchumi wa Tanzania.

Katika maelezo yake Mwakajoka alipokuwa akichangia makadirio ya bajeti ya Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na  Michezo kwa mwaka wa fedha 2019/20, alisema waandishi wa habari wamejaa hofu ya kuripoti mambo mbalimbali yakiwamo hali ya uchumi wa Tanzania.

Kutokana na hali hiyo alishauri waandishi wa habari waachwe huru ili waripoti mambo mbalimbali kwa maslahi ya umma.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles