“Anashukuru sana kwa kupewa mwaliko wa kuwa kocha wa Syria, lakini kwa sasa jambo hilo haliwezekani kwa kuwa anatafuta klabu ya kuitumikia nchini England,” alisema Mendes.
Mourinho mwenye umri wa miaka 53, alifukuzwa kazi na Chelsea kwa mara ya pili Desemba mwaka jana, ambapo kwa sasa inadaiwa kwamba kocha huyo kuna uwezekano mkubwa wa kuitumikia klabu ya Manchester United japokuwa kocha huyo amedai bado hajamalizana na United.
Ripoti za wiki iliyopita zilisema Mourinho ameanza kutafuta nyumba eneo la Cheshire jijini Manchester baada ya wawakilishi wake kufanya mazungumzo na klabu ya Manchester United.