24.2 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

MKUU WA CIA WA ZAMANI AONDOLEWA ULINZI

MAREKANI

Rais Donald Trump ameagiza kuondolewa ulinzi kwa aliyekuwa mkuu wa Shirika la Ujasusi la Marekani (CIA), John Brennan.

Rais Trump ametoa agizo hilo kwa madai kwamba Brennan ni mtu asiyeeleweka katika uadilifu na asiyefuata misingi.

Brennan alikaririwa akikosoa na kusema mkutano kati ya Rais Trump na Rais Vladimir Putin wa Urusi uliofanyika mwezi July mjini Helsinki, kwamba haukuwa na maana yoyote.

Vilevile aliandika kwenye ukurasa wake wa Twitter kuwa hatua hiyo ni jitihada za Rais Trump kudidimiza uhuru wa kujieleza na kuwaandama wakosoaji wa utawala wake.

Brennan amewataka raia wote wa Marekani kutilia mashaka jambo hilo na mwenendo huu wa rais, na kuwatahadharisha wataalamu na wana usalama kuwa makini na hatua hizi za Trump

Kwa upande wake Rais Trump, amekuwa akipuuza madai hayo na kusema kuwa ni jambo linalozushwa tu kwa maslahi ya kisiasa.

 

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles