24.2 C
Dar es Salaam
Tuesday, April 23, 2024

Contact us: [email protected]

Mbaroni kwa kumchoma moto mtoto

NA ALLAN VICENT 

JESHI la Polisi mkoani hapa linamshikilia  Salma Hassan, mkazi wa Kata ya Malolo katika Manispaa ya Tabora kwa tuhuma za kujeruhi kwa kumchoma moto mapajani mtoto mdogo   Johari (3) aache tabia ya kukojoa kitandani.

Kamanda wa   Polisi mkoani hapa, Emanuel Nley alisema mwanamke huyo amekamatwa kwa ajili ya uchunguzi wa tuhuma hizo na ikibainika  kahusika katika unyanyasaji huo atafikishwa mahakamani.

Alisema  awali ndugu wa karibu wa mtoto huyo walikuwa hawataki habari hizo zijulikane hivyo wakakaa kimya lakini   polisi walipata taarifa kutoka kwa wasamaria wema ndiyo maana mtuhumiwa huyo ameweza kukamatwa.

Shuhuda wa tukio hilo ambaye ni jirani na familia hiyo (ambaye hakupenda jina lake liandikwe gazetini) alieleza kuwa mtuhumiwa huyo anadaiwa kutenda kitendo hicho cha kinyama mara kwa mara.

Alidai   aligundua tatizo hilo Mei 5 mwaka huu baada ya kufika nyumbani kwa mtuhumiwa na kumbeba mtoto huyo ambaye  alikuwa akilalamika kwa maumivu makali na alipomhoji ndipo akagundua kufanyiwakitendo hicho.

“Nilipita nyumbani kwao nikambeba mtoto huyo lakini alikuwa analalamika kuwa anaumia kwenye mapaja.

“Nilipomuuliza amefanya nini akaeleza kuwa ana vidonda pajani kwamba  alichomwa moto na shangazi yake akome kukojoa kitandani,” alidai.

Alieleza kuwa mtoto huyo alidai kuwa shangazi yake alimchoma moto mapajani  aache tabia ya kukojoa kitandani.

Alisema hali hiyo ilimfanya   kwenda kutoa taarifa polisi.

Shuhuda huyo aliomba hatua za  sheria zichukuliwe  kukomesha vitendo vya namna hiyo ambavyo ni vya kinyama na ukatili mkubwa kwa watoto wadogo na hasa ikichukuliwa kuwa vinafanywa na  kinamama wasiojali.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles