25.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Matatizo ya uwekezaji mkubwa yaikumba Afrika Mashariki

Hali ya mazao ya Biashara na Mafuta Barani Afrika
Hali ya mazao ya Biashara na Mafuta Barani Afrika

Na Mwandishi Wetu,

Uchumi wa dunia umevia na hivyo kufanya miradi mipya ya rasilimali kuwa katika hali ya sintofahamu, ingawa wahusika wanajikaza kisabuni na kusema mambo bado ni shwari.

Ukweli ni kuwa miradi ya gesi na mafuta si kitu kwa sasa kwani bei ya bidhaa imeanguka vibaya na kuwa na thamani kama ya theluthi yake ya miaka mitatu iliyopita.

Habari toka Kampala zinasema kuwa uwezekano wa Uganda kusafirisha nje mafuta yake yanakabiliwa na matatizo ya kifedha kama ilivyo kwa Tanzania na Msumbiji. Habari hizo ni mwiba kwa wawekezaji  ingawa ni habari njema kwa   wenye  mitaji na wanaotafuta hisa kwenye kampuni za mafuta  kwani hununua inapokuwa bei chini na kuuza hisa bei inapokuwa juu.

Nchini Tanzania, Kampuni ya Statoil inayoongoza kwa uchimbaji mafuta na gesi nchini, imesema itachukua miaka mitano kujadili  faida za mafuta kwa nchi na haswa maudhui  ya taifa (local content) kwa mtambo wa kuchakata LNG.

Kutoka Uganda, Tullow Oil, Total  SA na CNOOC  wanatafuta  fedha za uwekezaji ikiwamo ya kujenga miundombinu ikiwamo bomba kutoka Hoima kule Uganda  hadi Bandari ya Tanga ambapo  itajengwa  mitambo ya kituo cha kujazia mafuta katika eneo la  Tongolani.

Kiasi cha Dola bilioni 4.0 zinahitajika   za kujenga kilomita 1430 kwa muda wa miaka mitatu ambapo Tanzania imepewa jukumu hilo baada ya ushindani na kuipiku nchi ya Kenya .

Mchambuzi wa Bloomberg Intelligence ya London, Will Hares, anasema shida kubwa kwa Uganda ni kwamba kila kitu ni kwa mara ya kwanza na hivyo ina hatari kubwa kiuwekezaji.

“Ratiba zinawezwa kukiuka na kuweka kila mtu kwenye wasiwasi na hivyo kufanya mradi uwe na gharama kubwa, kwani wadau wote wataathirika ikiwa  mradi utacheleweshwa,” anasema.

Uganda ina hazina ya mafuta inayokisiwa kufikia mapipa bilioni 1.7 katika Ziwa Albert  na Serikali inategemea kuanza uzalishaji wa mafuta mwaka 2021 na inategemea kupata mapato ya Dola bilioni 43 katika miaka 25 ya uendeshaji mradi.

Kuendeleza uzalishaji wa mafuta zinahitajika Dola bilioni 8 ingawa michoro ya kihandisi haijaanza kutengenezwa.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa George Cazenove,  msemaji wa Tullow,  zinasema Tullow inatakiwa ifanye uamuzi wa mwisho  wa kuwekeza inapofikia mwaka 2018 na ujenzi utakamilika ndani ya miaka mitatu,

Aina ya Kituo cha Mafuta kitakachojengwa Bandari ya Tanga kusafirishia mafuta ya Uganda
Aina ya Kituo cha Mafuta kitakachojengwa Bandari ya Tanga kusafirishia mafuta ya Uganda

na kuhimiza mradi kiwanja cha ndege kinachotegemewa kujengwa kwenye eneo la mradi kurahisisha mawasiliano. Kwa maelezo ya Robert Kasande, Mkuu wa Kitengo cha Mafuta cha Serikali ya Uganda katika mahojiano ya Novemba 10 mwaka huu, msemaji wa Total Ahlem Friga Noy na Msemaji  wa  CNOOC, Aminah Bukenya, hawakusema chochote walipoulizwa mipango yao ya uwekezaji.

Kwa ujumla, Waganda wamekuwa watatanishi kidogo kuhusu uendelezaji wa sekta ya mafuta ambapo imechukuwa takriban miaka 10 kutoa leseni, wakati Ghana ilichukua   miaka mitatu tangu ilpogundulika hadi kuanza uzalishaji mafuta.

Vilevile  Uganda ni kigeugeu kwani baada ya kuahidi kwa muda mrefu kuwa itaipa Kenya fursa ya kupitisha  bomba huko, ikabadili na kulipitisha Tanzania dakika za mwisho na hivyo ni jambo la kulizingatia na kutafakari kwa kina  kwani linaweza kujirudia.

Ujumbe wa Uganda uliofuatilia suala hilo, walifurahia namna Tanzania ilipolifikisha kwa marefu na mapana na kujua kweli ina nia na uwezo wa kukamilisha ujenzi kwa muda uliopangwa.

Kenya nayo inaonekana kukumbwa na matatizo ya uwekezaji katika mradi wake mkubwa wa LAPSETT kwa kukimbiwa na wawekaji wa Sudan Kusini na Ethiopia na hivyo kuvurugwa kwa mwelekeo wa mwenendo wa mradi huo, lakini tarehe  za utekelezaji wa mradi itabidi zipangwe upya kuzingatia mabadiliko hayo. Mapato ya Sudan kwa asilimia 95  ni mafuta na hivyo kudorora kwa bei kumeifanya taifa hilo changa kuchanganyikiwa.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles