Na CHRISTOPHER MSEKENA
IKIWA ni siku chache zimepita toka lebo ya Universal Music Group kumtunuku msanii Diamond Platnumz tuzo ya wimbo wake wa MARRY You kufikisha mauzo ya Platnum mara sita, msanii huyo amejikuta kwenye wakati mgumu baada ya kuwaita watoto wake (Tiffah na Nillan), mbegu.
Katika kile kilichoonekana kama ni kuwajibu wale wanaosema mtoto wake wa pili (Nillan) siyo wake, Diamond aliweka picha kwenye Instagram akiwa amewapakata watoto wake kuthibitisha kuwa wote ni wake kwa kuandika maneno yaliyopokewa kwa mitazamo tofauti.
Diamond Platnumz aliandika maneno ya Kiingereza yemye maana ya mbegu zangu, akimaanisha Tiffa na Nillan ni mbegu zake jambo ambalo lililofanya mashabiki wamjie juu kwa kutokuwa na lugha nzuri kwa wanawe.