25.2 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

Marekani yatoa picha jinsi ilivyomvamia Baghdadi, yamzika baharini kama Osama

WASHINGTON, MAREKANI

MAREKANI imetoa kanda ya video ambayo ni ya kwanza ikionyesha wanajeshi wakiwafyatulia risasi wanamgambo ardhini wakati walipokuwa wakikaribia nyumba ya aliyekuwa Kiongozi wa Islamic State, ISIS, Abu Bakr al- Baghdadi.

Picha hizo zinaonyesha kuwa kabla ya wanajeshi hao kuingia ndani ya nyumba hiyo Baghdadi alitorokea katika handaki na kujilipua.

Baada ya uvamizi huo nyumba hiyo iliharibiwa na silaha kali.

Zaidi Marekani imekiri kuzika mabaki ya mwili yake baharini kama ilivyokuwa kwa kiongozi wa kundi la kigaidi duniani la Al Qaeda, Osama Bin, Laden.

Akielezea jinsi walivyovamia makazi ya Baghidadi, Mkuu wa kitengo cha ulinzi Jenerali Kenneth Mckenzie, alisema kwamba jumba hilo lililoharibiwa lilikuwa kama eneo la kuegesha magari likiwa na mashimo mengi.

Jenerali McKenzie alisema kwamba watoto wawili walifariki na Baghdadi katika handaki hilo na sio watatu kama ilivyoripotiwa awali.

Hatahivyo hakuweza kuelezea maelezo ya rais Trump kwamba Baghdadi alikua akipiga kelele na kulia wakati alipokuwa akikaribia mauti yake.

”Alitambaa hadi katika handaki moja na watoto wawili wadogo na kujilipua huku wapiganaji wake wakisalia ardhini. Unaweza kuelewa ni mtu wa aina gani kupitia kitendo hicho” , aliuambia mkutano na wanahabari.

”Hayo ndiyo maelezo yangu ya kile alichokifanya. Sina uwezo wa kuthibitisha kitu kingine chochote kuhusu dakika zake za mwisho…Siwezi kuthibitisha hilo kwa njia moja ama nyingine”.

Jenerali Mckenzie alisema kwamba wanawake wanne – ambao walikuwa wakivalia fulana zilizojaa mabomu na mwanaume mmoja waliuawa ndani ya nyumba hiyo.

Alisema kwamba idadi kadhaa ya wapiganaji isiojulikana pia walifariki baada ya kuzifyatulia risasi ndege za Marekani.

“Nataka kuweka wazi kwamba licha ya shinikizo kali na kiwango cha juu cha shambulizi hilo kila juhudi zilifanywa ili kuzuia kuwaua raia wasio na hatia na kuwalinda watoto tulioshuku huenda walikuwa katika nyumba hiyo,” alisema.

Jenerali Mckenzie alithibitisha kwamba kiongozi huyo alitambuliwa kupitia vinasaba vya DNA, akiongezea kwamba sampuli zake zilikuwa katika faili tangu Baghdadi alivyohudumia kifungo katika jela moja ya Iraq mwaka 2004.

Alisema kwamba mabaki ya Baghdadi yalipelekwa katika kambi moja ya kuyatambua na baadaye yakazikwa baharini katika kipindi cha saa 24 baada ya kifo chake kulingana na sheria ya mizozo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles