24.4 C
Dar es Salaam
Tuesday, April 23, 2024

Contact us: [email protected]

Marekani yatoa masharti kuijenga upya Syria

WASHINGTON, MAREKANI

WAZIRI wa Mambo ya Nje wa Marekani, Mike Pompeo amesema nchi yake haitakubali kutoa msaada wowote wa ziada wa kuijenga upya Syria ikiwa vikosi vya Iran vitaendelea kuwepo nchini humo.

Akizungumza mbele ya kundi la wabunge wanaoiunga mkono Israel, Pompeo ameahidi ataendelea kushinikiza Iran itengwe na kuwekewa vikwazo vikali kabisa kuwahi kushuhudiwa.

“Jukumu la kuifukuza Iran linaangukia mikononi mwa Serikali ya Syria, ambayo ndiyo inayobeba dhamana ya kuwepo kwa wanajeshi wa nchi hiyo nchini humo.

“Ikiwa Syria haitohakikisha wanajeshi wa Iran wanaihama nchi hiyo, basi haitopokea hata dola moja kutoka Marekani,” alisisitiza Pompeo.

Hata hivyo, hakuzungumzia umuhimu wa kuondolewa pia kwa wanajeshi wa Urusi nchini humo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles