30.2 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

MAOFISA TBS WAFANYA UKAGUZI WA KUSHTUKIZA

NA MWANDISHI WETU- DAR ES SALAAM


MAOFISA wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS), wamefanya ukaguzi wa kushtukiza kwa wasambazaji wa bidhaa za viwandani na kuchukua sampuli na kuzihakiki ili kujiridhisha kama zinakidhi matakwa ya leseni walizopewa kwa ajili ya kutumia alama ya ubora.

Maofisa wa TBS walifanya ukaguzi Dar es Salaam juzi na kuchukua sampuli za nondo na mabati kutoka kwa Wakala wa bidhaa hizo, FMJ Hardware Ltd.

Akizungumza baada ya ukaguzi huo, Ofisa Viwango wa TBS, Joseph Ismail, alisema ukaguzi huo ni kwa mujibu wa taratibu za shirika hilo ili kuhakikisha wazalishaji waliopewa leseni ya kutumia alama ya ubora wanaendelea kufuata viwango vya ubora.

“Mojawapo ya kazi zetu ni kutoa leseni kwa wazalishaji, kwa hiyo tunafanya ukaguzi wa kushtukiza kwa wasambazaji wakubwa (mawakala) ili kuchukua sampuli na kuzipima katika maabara zetu kuona kama zinakidhi ubora tuliohakiki,” alisema.

Pia alisema wakitoa leseni ya ubora kwa wazalishaji viwandani, bidhaa zinazozalishwa hupelekwa kwa mawakala wanaowauzia wananchi, hivyo na wao wanafanya ukaguzi huo kujiridhisha kama waliopewa leseni hizo wanaendelea kufuata taratibu walizopewa.

Alisema wale wanaokiuka matakwa ya leseni wanapewa taarifa na kuchukuliwa

hatua za kisheria ikiwamo kuteketezwa kwa bidhaa hizo na ili kuepukana na usumbufu huo aliwataka wazalishaji kote nchini kuhakikisha wanazalisha bidhaa zinazokidhi matakwa ya leseni zao.

“Kwa hiyo lengo la ukaguzi huu ni kuzuia wazalishaji wasiingize sokoni bidhaa ambazo hazina ubora na mwisho kabisa kuwaepusha wasipate hasara kwa kulinda mitaji yao,” alisema.

Kwa upande wake, Ofisa Uhusiano wa TBS, Rhoida Andusamile, alisema ukaguzi huo unakusudia kuhakikisha bidhaa zinazozalishwa viwandani zinakidhi matakwa ya leseni wanazopewa.

“Shirika letu lipo kwa ajili ya kuwalinda walaji, ndiyo maana tunapita kwa wasambazaji wakubwa (mawakala) kuchukua sampuli ili kuzipima upya  kujiridhisha kama zina ubora ule ule wa kwanza tulioupima katika maabara wakati tunawapa leseni ya kutumia alama ya ubora ya shirika letu,” alisema.

 

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles