27.1 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Makocha wa Tanzania waikwepa Azam FC, Cioaba kurudi


SAADA SALIM, DAR ES SALAAM

Licha ya uongozi wa Azam FC kutangaza kusaka kocha mkuu wa kuifundisha timu yao hiyo lakini makocha wa Tanzania bado hawajawasilisha barua zao za maombi ya nafasi hiyo iliyokuwa ikishikiliwa na kocha, Hans der Van Pluijm.

Majina ya makocha na CV zao yaliyopokelewa na uongozin wa Azam wakiwania nafasi hiyo nio 10 ambao ni raia wa kigeni na wane kati yao walishawahi kufundisha timu za hapa nchini akiwemo kocha aliyewahi kuifundisha timu hiyo, Aristica Cioaba.

Mtendaji Mkuu wa Azam FC (CEO), Abdulkarim Amini (Popat), amesema hadi leo hawajapokea barua wala CV ya kocha yeyote kutoka Tanzania ila wamepokea majina 10 ya makocha kutoka nje ya nchi akiwemo aliyewahi kuifundisha timu hiyo.

“Bado hatujachagua kocha wa kuchukua nafasi ya Pluijm lakini tumepokea maombi ya makocha 10, huku wanne walishawahi kupita Tanzania wakiwemo Cioaba, Goran Kopunovic, Mosses Basena aliyewahi kuifundisha Simba na Leonard Neiva aliyewahi kuwa msaidizi wa Marcio Maximo wakati alipokuwa akiifundisha  Yanga.

“Kwa Cioaba kama atarudi ama la ni taarifa tu, kama ni kweli  itajulika lakini kwa sasa tunaendelea na mchakato wetu baada ya kumalizika kwa ligi, lolote linaweza kutokea, kikubwa tunahitaji mwalimu atakayeendana na malengo yetu,” amesema Amini.@

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles