31.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Majaliwa awaonya wakimbizi Katavi

WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa
WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa

Na MWANDISHI WETU, MPANDA

WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa, amesema wakimbizi waliopewa uraia wa Tanzania na kuutumia vibaya, watanyang’anywa uraia huo na kurudishwa walikotoka.

Kutokana na hali hiyo, amewataka raia hao wa Tanzania kuendelea kukumbushana juu ya umuhimu wa amani ili waendelee kuishi kama Watanzania wengine.

Majaliwa alitoa kauli hiyo jana alipokuwa akizungumza na waliokuwa wakimbizi wa Burundi ambao kwa sasa wamepewa uraia wa Tanzania wanaoishi katika Kata ya Katumba, Halmashauri ya Nsimbo, wilayani Mpanda, mkoani Katavi.

“Wakimbizi waliopewa uraia wameendelea kuingiza ndugu zao. Naagiza kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa ifanye ukaguzi katika kambi zote kwa sababu zimegeuzwa kuwa maficho ya kuwahifadhi watu wanaoingia nchini bila ya vibali.

“Hakikisheni mnachukua hatua kwa wote watakaoingiza watu kinyemela katika Kambi za Wakimbizi za Mishamo na Katumba. Pia msiruhusu watu kuleta silaha kwenye maeneo haya kwa sababu Tanzania watu wanaoruhusiwa kutembea na silaha ni askari tu,” alisisitiza Waziri Mkuu.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles