30.2 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

MAJALIWA ASISITIZA AMANI YA NCHI KUVUTIA WAWEKEZAJI

 


Na Mwandishi Wetu-DAR ES SALAAM

WAZIRI Mkuu Majaliwa Kassim Majaliwa amewaasa watanzania kulinda amani iliyopo kuvutia wawekezaji wengi nchinizaidi  miongoni mwa sifa za Tanzania ni utulivu ambao ni kichocheo kikubwa cha ukuaji uchumi.

Kauli hiyo aliitoa juzi Ikulu jijini Dar es Salaam wakati akitoa neno la shukrani kwa Mwenyekiti wa Mkutano wa 11 Baraza la Taifa la Biashaara Tanzania (TNBC) uliokutanisha wafanyabishara ambapo alisema uchumi unakua kwa kasi na wawekezaji wanavutiwa kuanzisha biashara mpya kutokana na hali ya utulivu.

“Kuna uhusiano mkubwa kati ya amani na ukuaji kiuchumi na ndiyo maana kuna mzungumzaji mmoja kutoka Arusha alisema watalii wameongezeka nchini na kipato kimeongezeka kwa kiwango kikubwa,” alisema

Majaliwa alimshukuru Rais Dk. John Magufuli ambaye alikuwa mwenyekiti wa mkutano huo kwa kutoa nafasi kubwa kwa wafanyabishara na sekta binafsi kuzungumza masuala yanayowakwaza ili serikali itoe majibu muafaka na kupatikana njia sahihi ya kuimarisha mazingira ya biashara nchini.

“Nashukuru ndugu rais ametoa majibu hapa hapa kwa baadhi ya malalamiko ya wafanyabiashara lakini naamini hawezi kumaliza yote hapahapa kwa sababu kuna mengine yanahitaji kujadiliana ndani ya vikao vyetu,” alisema Majaliwa.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles