31.7 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

Mahakama yawaachia huru askari wanane kesi ya kutorosha dhahabu Mwanza

Damian Masyenene, Mwanza

Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Mwanza, imewaachia huru na kuwafutia mashtaka askari wanane waliokuwa wanakabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi na utakatishaji fedha.

Askari hao walikuwa na mashtaka 12 yakiwamo ya  uhujumu uchumi, kuomba na kupokea rushwa ya Sh milioni 700, kuisababishia hasara Serikali na utakatishaji fedha ambapo walioachiwa ni pamoja na Koplo Dani Kasara, Matete Misana, Konstebo Japhet Kuliko, Maingu Sorry, Alex Mkali, Timoth Paul, David Ngelela na Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP), Moris Okinda aliyekuwa kiongozi wa askari hao na mshtakiwa wa kwanza kwenye kesi hiyo.

Uamuzi huo umetolewa leo Alhamisi Julai 18,  na Hakimu Mkazi wa Mkoa wa Mwanza, Rhoda Ngimilanga aliyekuwa anasikiliza kesi hiyo, ambapo amesema kutokana na ombi lililowasilishwa na Mkurugenzi Mkuu wa Mashtaka (DPP) kupitia kwa Wakili wa upande wa mashtaka, Castus Ndamgoba la kutokuwa na nia ya kuendelea na shauri hilo.

Washtakiwa hao ni miongoni mwa wafungwa wengine zaidi ya 200 kutoka magereza mbalimbali waliofutiwa mashtaka na kufutiwa vifungo vyao jana baada ya Rais John Magufuli kufanya ziara ya ghafla katika Gereza la Butimba, mkoani Mwanza juzi.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles