24.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Mahakama yamhalalisha Lipumba uenyekiti CUF

Kulwa Mzee, Dar es Salaam

Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imetupilia mbali shauri lililofunguliwa dhidi ya Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Lipumba kuhusu kuhoji uhalali wake.

Uamuzi wa shauri hilo namba 23 la mwaka 2016, umetolewa leo Jumatatu Machi 18 asubuhi, mbele ya Jaji Benhajj Masoud.

Akitoa uamuzi huo, Jaji Masuod amesema baada ya mahakama kupitia hoja za pande zote mbili imebaini kwamba katika maombi kuna makosa ya kisheria ambapo Bodi ya Wadhamini ya CUF haikutoa idhini kwa Katibu Mkuu wa chama hicho, Maalim Seif Sharif Hamad, kusaini kiapo kilichowasilishwa mahakamani.

Pia alisema hakuna ushahidi kwamba Maalim Seif alipewa kibali cha kufanya hivyo.

Jaji Masoud amsema kwamba Msajili alikuwa na mamlaka ya kufanya kile alichokifanya kumrejesha Lipumba ndani ya CUF.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles