23.8 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

LUKUVI AFUTA HATI 15 ZA VIWANJA VYA MWINGEREZA

 WAZIRI wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi
WAZIRI wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi

Na JUDITH NYANGE – MWANZA

WAZIRI wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi amefuta  hati za viwanja 15 vilivyokuwa vinamilikiwa na Hermant   Patel na kurejesha umiliki wake kwa serikali.

Inaelezwa kuwa viwanja hivyo vilipatikana kwa  njia ya udanganyifu.

Akizungumza na waandishi wa  habari   Mwanza jana, Lukuvi alisema anaishukuru ofisi ya ardhi Kanda ya Ziwa kwa kutekeleza agizo la kufuta umiliki wa hati 15 za Patel.

Alisema mtu huyo  alipata hati hizo  kwa njia ya udanganyifu kwa kutumia hati ya uraia pacha wa Tanzania na Uingereza.

Waziri alisema awali ilidhaniwa  Patel anamiliki hati tano za viwanja lakini kwa kushirikiana na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(TAKUKURU) imegundulika  ana hati 15 alizozipata kwa njia ya udanganyifu kwa kuwa na uraia wa nchi mbili.

“Patel ni raia wa Uingereza kwa sheria za nchi hii haziruhusu raia wa kigeni kumiliki ardhi, viwanja vyote  15 ambavyo alikuwa anavimiliki  vimerudi serikalini.

“Leo  nimeagiza ekari 30 alizokuwa anamiliki  katika  Halmashauri ya Wilaya ya Busega mkoani Simiyu vikabidhiwe kwa mkurugenzi   vitumike kwa shughuli za maendeleo ikiwamo uchimbaji wa mabwawa.

“Viwanja vingine vilivyobaki kwa kuwa vipo mwambao wa Ziwa Victoria  vitangazwe ili vipate wawekezaji.

“Viwanja vingine vilivyobaki ambavyo Patel alikuwa anavimiliki katika mikoa ya Mwanza,  Geita na Simiyu nimevirudisha  katika kamati ya ugawaji wa ardhi ya taifa  vipigwe mnada   serikali ipate  fedha.

“TAKUKURU wataendelea na hatua nyingine za kisheria ikiwemo kumfikisha mahakamani,” alisema Lukuvi

Lukuvi aliwaonya watu wote wenye tabia kama ya Patel ya kutumia hati za kuishi nchini zenye uraia  wa nchi mbili, ambao walifanya udanganyifu na wanamiliki ardhi kama raia wa Tanzania wajisalimishe vinginevyo watashughulikiwa na kunyang’anywa ardhi wanazozimiliki.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles