Na MWANDISHI WETU
-DAR ES SALAAM
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kinaonekana kuvurugwa kimkakati kufikia malengo yake ya kisiasa kuelekea Ikulu.
Tukio jipya na ambalo limeingia katika orodha ya mambo ambayo yanaonekana kutibua mipango ya kisiasa ya chama hicho kikuu cha upinzani kushika dola, ni uamuzi wa kushtukiza alioufanya aliyekuwa mgombea wao wa urais mwaka 2015, Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa kurejea CCM juzi jioni.
Kabla ya kurejea CCM, Lowassa alijiunga Chadema baada ya jina lake kukatwa kimizegwe katika mchakato wa kuwania urais mwaka 2015.
Lowassa ambaye katika uchaguzi huo wa 2015 alitoa upinzani mkali kwa Rais Dk. John Magufuli akishika namba mbili kwa wingi wa kura, kurejea kwake CCM kunakuja katika wakati ambao Chadema inapitia katika hali tofauti na ngumu kisiasa.
Ameondoka Chadema katika wakati ambao …
Kwa habari zaidi jipatie nakala yako ya gazeti la MTANZANIA.