31.7 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

KWAYA YA AICT CHANG’OMBE KUADHIMISHA MIAKA 30

Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Kwaya ya Kanisa la African Inland Church (AICT) Chang’ombe maarufu CVC ya jijini Dar es salaam inatarajia kufanya maadhimisho ya miaka 30 tangu kuanzishwa kwake.

Katibu Mtendaji wa CVC, Hosea Kashimba amesema, tukio hilo litakutanisha kwaya zote maarufu zikiwamo, Kinondoni Revival, Tumaini Shanilieni ya Arusha, Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Uinjilisti Kijitonyama, KKKT Msasani na nyingine nyingi.

“Maadhimisho hayo yataanza Aprili 28, mwaka huu kwa kuweka jiwe la msingi wa Kituo cha Mikutano cha kwaya hiyo eneo la Mtoni Kijichi jijini Dar es Salaam,” amesema Kashimba.

Pamoja na mambo mengine, Kashimba amesema katika tukio la kuweka jiwe la msingi la kituo hicho linatarajiwa kuwekwa na Askofu wa Kanisa hilo Dayosisi ya Pwani, Charles Salalah.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles