33.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

KIZIMBANI KWA KULAWITI MTOTO WA MIAKA 12

b897c623

JOHANES RESPICHIUS Na ATUPENDA GEOFREY (MPS)-DAR ES SALAAM

MKAZI wa Tandale Kinondoni, Dar es Salaam, Ramadhani Ibrahim (32), amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Wilaya Kinondoni kwa tuhuma za kumlawiti mtoto wa kiume mwenye umri wa miaka 12 (jina tunalo).

Akisomewa shtaka lake mbele ya Hakimu Mkazi, Boniface Lihamwike, Mwendesha Mashtaka, Tumaini Mfikwa, alidai mtuhumiwa alifanya kosa hilo Novemba 18, mwaka jana maeneo ya Tandale.

“Novemba 18, mwaka jana, maeneo ya Tandale, mtuhumiwa Ramadhani kwa makusudi ulimlawiti mtoto wa kiume mwenye umri wa miaka 12, huku ukijua kufanya hivyo ni kinyume cha sheria,” alidai Mfikwa.

Baada ya kusomewa shtaka hilo, mtuhumiwa alikana kutenda kosa hilo na kuambiwa shtaka hilo linadhaminika awe na wadhamini wawili ambao walitakiwa kusaini bondi ya Sh 2.5.

Kesi hiyo, iliahirishwa hadi Januari 23, mwaka huu itakapotajwa tena mahakamani hapo kwa kusikilizwa kwa mara ya kwanza na mtuhumiwa alirudishwa rumande kutokana na kushindwa kukidhi masharti ya dhamana.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles