25.2 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

Kisa mapaparazi, Kylie apata ajali

kylie-jennerLOS ANGELES, MAREKANI

MPENZI wa mkali wa muziki wa hip hop nchini Marekani, Tygar, Kylie Jenner, amesema hana urafiki na waandishi wa habari nchini humo kwa kuwa walimsababishia ajali.

Mrembo huyo amesema hana amani kila akiwa katika matembezi yake ya kawaida kwa kuwa waandishi wa habari wanamzonga mara kwa mara.

Hata hivyo, mwezi uliopita alikutana na waandishi wa habari akaanza kuwakimbia na gari yake na kusababisha ajali wakati anawakimbia waandishi hao.

“Siwezi kuwa na urafiki na waandishi wa habari, wananifuatilia sana, mwezi uliopita nilipata ajali mbaya ya gari kwa kuwakimbia wao, hivyo ninawachukia kwa kiasi kikubwa kwa kuwa hawana heshima, lakini ninakubali kile wanachokifanya ila wanatakiwa kuniheshimu ili tuheshimiane,” alisema Kylie.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles