31.2 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

KISA GIGI HADID, ZAYN AUZA NYUMBA

LONDON, UINGEREZA



MWIMBAJI maarufu wa muziki nchini Uingereza, Zayn Malik, ametangaza kuuza nyumba yake iliyopo Kaskazini mwa Uingereza na kuhamia Jiji la New York nchini Marekani, kwa ajili ya kumfuata mpenzi wake, Gigi Hadid.

Nyumba hiyo inasemekana ina vyumba vitano vya kulala, lakini ameamua kuiweka sokoni ili kwenda kuishi pamoja na mrembo huyo raia wa Marekani.

Zayn mwenye miaka 25, alikaa miezi 12 jijini New York na mrembo huyo, hivyo ameamua kufanya maamuzi ya kutaka kuhamia moja kwa moja nchini humo baada ya uhusiano wa wawili hao kuendelea kushamiri kwa kasi.

Gazeti la The Sun limeripoti kuwa Zayn amekuwa na furaha sana kuishi nchini Marekani kwa sasa na anaamini huu ni muda sahihi wa kuuza nyumba hiyo na kukimbilia Marekani anakotumia muda mwingi kuishi.

Thamani ya nyumba hiyo imetajwa kuwa pauni milioni 3.5 ambazo ni zaidi ya Sh bilioni nane za Kitanzania.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles