29.2 C
Dar es Salaam
Wednesday, April 24, 2024

Contact us: [email protected]

KIBA AFURAHIA COKE STUDIO

NA MWANDISHI WETU

MKALI wa muziki wa Bongo Fleva nchini, Ali Kiba, amesema moja ya mafanikio ambayo anajivunia kwa mwaka huu ni kushiriki tena onyesho la Coke Studio.

Kiba, ambaye amefanya kolabo na mwimbaji wa Nigeria, Patoranking, amesema kushiriki msimu huu wa tano wa Coke Studio kutamfanya aongeze idadi kubwa ya mashabiki.

“Kushiriki katika onyesho hili linaloandaliwa na kampuni kubwa ya vinywaji ya Coca Cola pamoja na kushirikiana na Patoranking, kunanifanya niongeze mashabiki na umaarufu wangu kuongezeka,” alisema Kiba.

Alisema onyesho la Coke Studio linadhihirisha kuwa Bongo Fleva inazidi kukua na kupata umaarufu sehemu mbalimbali barani Afrika kutokana na jinsi linavyofuatiliwa na idadi kubwa ya mashabiki.

Pia Kiba aliwapongeza wasanii wenzake kutoka Tanzania ambao wamepata nafasi ya kushiriki onyesho hilo la Coke Studio linaloonyeshwa kila Jumamosi kwenye televisheni ya Clouds, ambapo wasanii hao ni Rayvanny, Izzo Bizness na Nandy.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles