NEW YORK, MAREKANI
NYOTA wa filamu nchini Marekani, Kevin Hart, ameingia kwenye wakati mgumu baada ya mke wake Eniko Parrish, kuomba maneno ya siri ‘Passward’ kwenye mitandao yake yote ya kijamii ili kudumisha upendo kwenye ndoa yao.
Wiki chache zilizopita msanii huyo alikuwa na mgogoro na mke wake, baada ya kuchepuka wakati huo ana ujauzito na wanatarajia mtoto hivi karibuni.
Baada ya kumaliza mgogoro huo, Eniko amemwambia Hart kuwa anatakiwa kumwachia huru kwenye mitandao yote ya kijamii kuingia wakati wowote kuangalia mambo yake.
Kwa mujibu wa mtandao wa TMZ, msanii huyo amekubali kumwachia wazi maneno yake yote ya siri kwenye mitandao ili kumuonesha kuwa anampenda.