27.2 C
Dar es Salaam
Tuesday, April 16, 2024

Contact us: [email protected]

Kevin Hart aomba tena radhi

NEW YORK, MAREKANI

MCHEKESHAJI maarufu nchini Marekani, Kevin Hart, ameomba tena radhi kwa kauli yake ya kuwazungumzia vibaya watu wanaoshiriki tendo la jinsi moja.

Msanii huyo ambaye aliteuliwa kuwa mshereheshaji kwenye tuzo za Oscar ambazo zinatarajiwa kufanyika Februari 25 mwaka huu, lakini kutokana na kauli za kuwazungumzia mashoga akaondolewa nafasi hiyo.

“Nitaendelea kuyasema haya kwa ajili ya kuacha kila kitu kikienda sawa sawa, nataka kuweka wazi kuwa, sina tatizo na watu wanaoshiriki matendo ya jinsia moja, nataka kila mmoja ajisikie huru na furaha.

“Nadhani maneno yangu hayakuwa na maana mbaya, lakini nilieleweka vibaya na ndio maana natumia muda mwingi kuweka sawa kwa kuomba radhi kwa kila mmoja ambaye aliguswa na maneno hayo,” alisema Kevin Hart.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles