30.2 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

Keisha: Sitamani kuzaa tena

K-Sher 2NA SHARIFA MMASI
BAADA ya mashabiki wake kumtaka aongeze mtoto wa tatu, msanii wa Bongo Fleva, Khadija Shaban (Keisha), ameibuka na kuweka wazi kwamba hana mpango wa kuzaa tena kwa sasa.
Keisha aliliambia MTANZANIA kuwa, sababu kubwa inayomfanya asitamani kuongeza mtoto kwa sasa ni kutokana na kuwa na watoto wawili wa kiume wenye umri mdogo.
“Najua watu wengi wanapenda watoto na hata mashabiki wangu wanatamani sana niendelee kuzaa, kiukweli bado nahitaji kulea madume yangu, kwani umri wao bado ni mdogo sana,” alisema Keisha.
Mtoto wa kwanza wa msanii huyo ana miaka minne na wa pili ana mwaka mmoja.
“Kama nitabeba ujauzito mwingine kwa sasa mimi na baba yao tutakuwa hatuwatendei haki hawa watoto wetu, wanahitaji muda wa kukua zaidi ndipo tufikirie kuongeza wenzao wengine,” alisema Keisha.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles