27.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Kabendera, akina Kaburu wamwandikia DPP kujadiliana namna ya kumaliza kesi zao

KULWA MZEE-DAR ES SALAAM

MWANDISHI wa Habari Erick Kabendera,  aliyekuwa Rais wa Klabu ya Simba, Evans Aveva na Makamu wake Godfrey Kaburu, wameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa, wameanza majadiliano na Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP) ya namna ya kumaliza kesi zao.

Hayo yalibainishwa jana mahakamani hapo kwa nyakati tofauti mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Augustine Rwizile ambapo Wakili Jebra Kambole alieleza kwa niaba ya Kabendera.

Wakili wa Serikali Mwandamizi, Wankyo Simon alidai kesi hiyo ilipangwa kwa ajili ya kutajwa na upelelezi haujakamilika.

Baada ya Wankyo kueleza hayo, Wakili wa utetezi Kambole aliijulisha Mahakama taarifa ya mteja wake kuandika barua  kwa mujibu wa kifungu namba 194A(2) cha sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai kama ilivyofanyiwa mareje mwaka 2019.

Akijibu Wakili Wankyo alidai ni kweli jambo hilo limefanyika na kwamba  Kabendera ameandika barua na ipo katika mchakato na watakapokuwa wamekamilisha wataitaarifu Mahakama.

Baada ya kusikiliza hoja hizo, Hakimu Rwizile aliahirisha Kesi hiyo hadi Oktoba 24, kwa ajili ya kutajwa. Na kama kutakuwa na chochote kabla ya tarehe Jamhuri wataiarifu Mahakama.

Kabendera anakabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi yenye mashtaka matatu likiwemo la utakatishaji wa zaidi ya Sh milioni 173.

Katika shtaka la kwanza ilidaiwa katika kipindi hicho, Kabendera alijihusisha  na mtandao wa kihalifu kwa kutoa msaada kwa genge la uhalifu kwa nia ya kujipatia faida.

Shtaka la pili ilidaiwa katika kipindi hicho, bila ya sababu, alikwepa kodi ya Sh. 173,247,047.02 ambayo ilitakiwa ilipwe Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Katika shtaka la tatu, kabendera anadaiwa kutakaisha Sh 173,247047.02 huku akijua fedha hizo ni mazalia ya kosa la kujihusisha na genge la uhalifu na utakatishaji fedha.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles