31.2 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

JPM: Ole wenu wataalamu mnaotumika

Na ELIZABETH HOMBO-DAR ES SALAAM


RAIS John Magufuli amewashukia wataalamu wa mazingira walioandaa ripoti kuhusu ujenzi wa mradi wa umeme wa Stiegler’s Gorge, kwa kutoa ripoti aliyoiita ya ovyo.

Amesema wataalamu hao katika ripoti yao walipendekeza ili mradi huo ujengwe wafanyakazi wote watakaokuwa wanafanya kazi katika eneo hilo lazima wawe wanajisaidia kilomita 10 kutoka ulipo mradi.

Alisema katika pendekezo jingine,  wataalamu hao waliandika kwamba kitu chochote kinachoingia katika eneo hilo lazima kipimwe na kwamba gari likiharibika katika eneo hilo lisitengenezewe hapo.

Rais alitoa kauli hiyo   Dar es Salaam jana wakati akizindua barabara ya  juu (fly over) kwenye makutano ya barabara za Nyerere na Mandela eneo la Tazara.

Barabara hiyo imejengwa na kampuni ya Sumitomo ya Japan na ina urefu wa kilomita moja, ikiwa  imegharimu Sh bilioni 106.

“Mikwamo yote hii inayowekwa ya mazingira baadhi imewekwa na Watanzania wenzetu, tunawaoita wataalamu waliozaliwa Tanzania na wengine weusi kuliko hata mimi.

Kwa habari zaidi jipatie nakala yako ya gazeti la MTANZANIA.
- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles