24.2 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

JK mkuu mpya UDSM

Jakaya-KikweteNa Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

RAIS Dk. John Magufuli amemteua Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Jakaya Kikwete kuwa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Taarifa iliyotolewa   na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue   Dar es Salaam jana ilieleza kuwa uteuzi huo ulianza Januari 17 mwaka huu.

Nafasi hiyo iliachwa wazi  Febuari 22, 2014 baada ya kifo cha aliyekuwa Mkuu wa Chuo hicho, Balozi Fulgence Kazaura   aliyeshika wadhifa huo kwa vipindi viwili vya miaka minne.

Balozi Kazaura kwa mara ya kwanza aliteuliwa 2005 baada ya kifo cha Paul Bomani ambaye alishika wadhifa huo kuanzia 1993.

Kuteuliwa kwa Kikwete   kumemfanya afuate nyayo za marais wa wastaafu waliopita; Ali Hassan Mwinyi, Mkuu wa Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Kampala (KIU) na Benjamin Mkapa ambaye ni Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).

 

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles