26.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

JANET AMTEMBEZA MTOTO KWA MASHABIKI

CALIFORNIA, MAREKANI

NYOTA wa muziki wa Pop nchini Marekani, Janet Jackson, ameanza kumtembeza mtoto wake kwa mara ya kwanza kwa mashabiki wake.

Msanii huyo mwenye umri wa miaka 51, kwa mara ya kwanza juzi alionekana akiwa mitaa ya California akiwa amembeba wazi mtoto wake, Eissa, ili mashabiki wamwone.

Mtoto wake huyo wa kwanza alizaliwa Januari mwaka huu na kumfanya Janet apumzike kufanya muziki kwa mwaka mmoja, lakini tayari ameweka wazi kuwa yupo tayari kuanza ziara zake.

“Najua mashabiki wangu wamenimisi sana, ila nataka kuwatoa wasiwasi na kuwaambia kwamba nipo njiani kuja kuwapa burudani, nilikuwa nasubiri mwanangu akue na nadhani sasa ni wakati sahihi wa kurudi kwa mashabiki,” alisema Janet.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles