30.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

JAMMEH AIKAUSHA HAZINA YA GAMBIA

Jammeh3
Yahya Jammeh akiondoka nchini Gambia

Aliyekuwa Rais wa Gambia, Yahya Jammeh, anasemekana kuondoka madarakani na zaidi ya dola za kimarekani milioni 11 kutoka katika hazina ya serikali.

Hayo ni kwa mujibu wa Mshauri maalumu wa Rais wa Gambia Adama Barrow, Mia Ahmad Fatty ambaye aliongea na waandishi wa habari katika mji mkuu wa Senegal Dakar.

Fatty aliongeza kuwa wataalamu wa masuala ya fedha wanatathmini kujua ni kiasi gani kwa sasa kimepotea.

Amesema Gambia kwa sasa ina tatizo kubwa kifedha kwa hazina yake kutokuwa na kitu.

Pamoja na hilo, kwa sasa Rais Barrow amekuwa akifanya kazi na timu ya wataalamu wa masuala ya fedha na wengine kutoka Benki kuu ya nchi hiyo kupata kiasi halisi kilichopo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles