30.2 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

JALADA KESI YA VIGOGO SIX TELECOM LAKWAMA KWA DPP

Patricia Kimelemeta na Maneno Selanyika, Dar es Salaam

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imeutaka upande wa mashtaka kuharakisha upelelezi wa kesi ya utakatishaji fedha inayowakabili vigogo wa Kampuni ya Six Telecoms Limited akiwamo Wakili maarufu Dk. Ringo Tenga.

Washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni Mkurugenzi wa zamani wa Benki ya Rasilimali (TIB) Peter Noni, Mhandisi na Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni hiyo, Hafidhi Shamte, Mkuu wa fedha wa kampuni hiyo, Noel Chacha.

Hakimu Mkazi Mkuu wa mahakamani hiyo, Thomas Simba amesema hayo baada ya Wakili wa Serikali Mwandamizi Mutalemwa Kishenyi, kuieleza mahakamani hiyo kuwa upelelezi bado haujakamilika.

Kishenyi alidai jalada la vigogo hao lipo mikononi mwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) na kuiomba mahakamani hiyo kupanga tarehe nyingine Kwa ajili ya kutajwa.

Upande wa utetezi ukiongozwa na Wakili Alex Mushumbusi ulidai kuwa wakati ujao upande wa mashaka uje na sababu za msingi na kuieleza mahakama upelelezi ulipofikia.

Hata hivyo, Hakimu Simba amesema ifike mahali upande wa mashtaka uharakishe upelelezi ili washtakiwa hao kama kufungwa wafungwe.

Amesema sababu zinazotolewa mahakamani hapo za kudai upelelezi haujakamilika itafika wakati zitakwisha kwa sababu upande wa mashaka ndiyo unaounganisha mahakama na DPP.

“Sisi hatuwezi kumuona DPP bali tunaunganishwa na ninyi (upande Wa mashtaka), kwa hiyo mnapaswa kukamilisha upelelezi ili washtakiwa kama ni kufungwa wafungwe,” amesema Hakimu Simba.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Aprili 20, mwaka huu kwa ajili ya kutajwa.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles