24.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

JAIVAH AMTAMANI VANESSA MDEE

NA CHRISTOPHER MSEKENA

MSANII wa Bongo Fleva anayefanya vizuri kwa sasa na wimbo wa Ngifuna Wena, Sebastian Charles ‘Jaivah’, amesema wasanii wa kike nchini wanatofautiana na ndio maana anatamani kufanya kazi na Vanessa Mdee.

Akizungumza na MTANZANIA jana alipotembelea ofisi za gazeti hili Dar es Salaam, Jaivah alisema Vanessa Mdee ni mfano wa kuigwa na wasanii wengine wa kike kwani anaweza kufanya muziki wa aina yoyote na mashabiki wakaendelea kupenda kazi zake.

“Natamani kufanya kazi na wasanii wote wa kike kwa sababu kila mmoja ana ladha yake, ila ningependa kuanza na Vanessa Mdee kwa sababu anaweza kufanya aina ya muziki ninaofanya,” alisema msanii huyo anayetumia Lugha ya Kizulu kwenye nyimbo zake.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles