31.7 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

Himid ahamishia kambi kwa Kichuya Misri

Mohamed Kassara -Dar es salaam

KIUNGO mkabaji Himid Mao ameungana na Mtanzania mwenzake, Shiza Kichuya kuichezea  klabu ya ENPPI,  baada ya kujiunga nayo kwa mkataba wa miaka miwili akitokea Petrojet iliyoshuka daraja.

Petrojet imeshuka daraja ikitoka Ligi Kuu Misri hadi Ligi Daraja la Kwanza, baada ya kumaliza nafasi ya 16, miongoni mwa  timu 18, ikimaliza na pointi 35, baada ya kucheza michezo 34.

Timu  nyingine zilizoshuka daraja ni El Dakhleya na Nogoom.

Himid ambaye ni nahodha msadizi wa kikosi cha Taifa Tanzania ‘Taifa Stars’, alijiunga na Petrojet Juni mwaka jana akitokea Azam FC ya hapa nchini.

Himid ameungana na nyota mwenzake katika kikosi wa Stars, Kichuya ambaye anaichezea klabu hiyo kwa mkopo, akitokea klabu ya Pharco inayoshiriki Ligi Daraja la Pili nchini humo.

Kichuya alijiunga na Pharco Februari mwaka huu akitokea Simba, kabla ya kutolewa kwa mkopo kwenda  ENPPI, ambapo alianza kuichezea timu katika mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Al Alhly uliomalizika kwa kuchapwa mabao 2-1.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles