30.2 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

HECHE AKAMATWA KWA UCHOCHEZI, MATIKO ASAKWA

Na Mwandishi wetu

MBUNGE wa Tarime Vijijini, (Chadema) John Heche anadaiwa kushikiliwa na Jeshi la Polisi Tarime kwa madai ya kutoa kauli bungeni ya kuhamasisha wananchi kuzuia shughuli za Kampuni ya uchimbaji madini ya Acacia, Nyamongo North Mara.

Taarifa iliyotolewa jana na Ofisa Habari Chadema, Tumaini Makene ilieleza kuwa, Heche alikamatwa jana huku Mbunge wa Tarime Mjini kupitia chama hicho, Esther Matiko akisakwa na jeshi hilo.

“Jeshi hilo linadai Heche kupitia mkutano wa hadhara alisema atapeleka hoja bungeni ili bangi ihalalishwe kuuzwa nje ya nchi, polisi wanasema kauli hiyo inachochea ulimaji bangi,” alisema Makene.

Makene alisema Matiko anasakwa ili kuunganishwa katika madai hayo kuwa alitoa kauli katika mkutano huo zinazochochea kilimo cha bangi.

Alisema jeshi hilo linashikilia simu za Heche na kwamba limeagiza simu nyingine iliyopo Dar es Salaam kwenye matengenezo ipelekwe mkoani humo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles