25.2 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

Halmashauri 12 zapewa ruzuku ya Sh bilioni 137

Na Mwandishi wetu

-Dodoma

SERIKALI imezipatia halmashauri 12 nchini ruzuku ya Sh  bilioni 137 kwa ajili ya kutekeleza miradi 15 ya  mkakati   kuongeza mapato ya ndani.

Katibu Mkuu na Mlipaji Mkuu wa Serikali, Doto James na wakurugenzi wa halmashauri hizo, walitia saini mkataba wa makubaliano hayo   Dodoma jana.

James alizitaka halmashauri  zilizopata fedha hizo kutumia fedha kwa malengo yaliyokusudiwa .

Alionya   hatua kali za  sheria zitachukuliwa kwa watendaji watakaokiuka makubaliano yaliyomo kwenye mkataba wa makubaliano.

“Maofisa masuuli mhakikishe mnafuata na kuzingatia Sheria ya Bajeti Namba 11 ya Mwaka 2015 na kanuni zake, ambayo pamoja na mambo mengine inasisitiza juu ya matumizi bora ya fedha kwa shughuli zilizoidhinishwa” alisema James.

Alisema  Serikali ilipoanzisha utaratibu huo haikuwa inatania wala kufanya mazingaombwe, inayo dhamira ya dhati ya kuzijengea uwezo halmashauri zijitegemee kwa uchumi na kutoa huduma bora kwa wananchi badala ya kutegemea ruzuku ya Serikali Kuu.

Aliwahakikishia wadau kuwa fedha hizo zipo na kuzitaka halmashauri zichangamkie fursa hiyo kwa ukamilifu.

Miradi inayotarajiwa kutekelezwa inahusisha masoko ya kisasa, kiwanda cha kusindika korosho, uendelezaji wa fukwe ya Oysterbay  na maegesho ya malori, iliyopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, Kigamboni, Tanga, Kibaha, Bagamoyo, Mwanza, Tarime, Hanang, Iringa na Biharamulo.

Kamishna wa Bajeti wa Wizara ya Fedha na Mipango,  Mary Maganga alisema awamu ya pili ya miradi ya  mkakati kwa Mamlaka za Serikali za Mitaa miradi iliyokidhi vigezo ni  15 yenye thamani ya Sh bilioni 137.38.

  Naibu Katibu Mkuu,   Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa-Tamisemi, Dk. Doroth Gwajima, aliipongeza Wizara ya Fedha na Mipango kwa kufanikisha upatikanaji wa fedha ambazo zitachochea miradi ya maendeleo katika halmashauri nchini.

Dk. Gwajima, alizitaka halmashauri zilizofanikiwa kusaini mikataba hiyo  kuhakikisha  zinazingatia lengo la mkataba huo na kutekeleza miradi kwa muda mwafaka na viwango vilivyoainishwaa na kwamba ufuatiliaji wa miradi hiyo utakuwa ni wa kiwango cha juu.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles