30.2 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

GRAPHEX MINING YAONGEZA HAZINA YA GRAFITI MTWARA

Na Joseph Lino, Dar es Salaam

Kampuni ya Graphex Mining imetangaza kuwa kuna  ongezeko  la asilimia 80 ya madini ya grafiti  katika mradi wa Chilalo uliyopo Nachingwea  nchini Tanzania.

Mradi wa Chilalo sasa utakuwa na tani milioni 16.9 za grafiti zenye kiwango cha graphitic carbon asilimia 10.2 na pamoja na tani milioni 5.2  zlizothibitishwa na tani milioni 11.7 haijathibitishwa kamili (inferred).

Ongezeko hilo  linafuatiwa baada kukamilika uchimbaji wa shimo 13 lenye mita 1 365.

Mkurungezi wa Gaphex, Phil Hoskins, alisema kuongezeka  kwa hilo  shimo katika mradi wa Chilalo inathibitisha  kuweko kwaa grafiti bora eneo hilo.  

"Kuongezeka kwa rasilimali ya madini inatarajia kuongeza maisha ya mradi  huo na kuboresha uchumi, haya ni matokeo bora yatakayosaidia katika mbinu za masoko  na maendeleo ya Chilalo ambayo yanatarajiwa kuleta matokeo mazuri kwa wanahisa,” alisema.

Hoskins alisema  mradi umetoa thamani ya umuhimu wa uwezo kuendelea na uchimbaji katika mradi wa Chilalo na habari hizi zitakaribisha  fedha za uendeshaji wakati mazungumzo yanaendelea.

Mradi wa Chilalo unakadiriwa kuwa na mtaji wa uendeshaji wa dola milioni  74 ambao utaweza kuzalisha tani 69,000 kwa mwaka kwa kipindi cha miaka 10.

Nayo Kampuni ya Volt Resources hivi karibuni ilitangaza kuwa  kampuni binafsi ya maabara kutoka German Metallurgical Laboratory ilithibitisha kuwepo kwa grafiti bora katika mradi wa Namangale uliopo mkoani Mtwara.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles