27.5 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

Array

Familia ya askofu yamwangukia Rais Magufuli

Na KENNETH NGELESI-MBOZI

FAMILIA ya Askofu Mulilege Mkombo Ambindwile Kameka wa Kanisa la ‘House of  Preyer Shield of  Faith Christian Church’  imemuomba Rais Dk.John Magufuli kuingilia kati na tatizo na kiongozi huyo ambaye kwa sasa inadaiwa yupo mahabusu tangu Januari mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa jana,  baba mzazi wa askofu huyo, Ambilikile Kameka, alisema anaiomba Serikali ya Rais Magufuli imnusuru kiongozi huyo wa kiroho.

Mchungaji Mwaipungu alisema askofu wao alikamatwa Jenuari 17,  mwaka huu Jijini Dar es Salaam, kwa hutuma za mashaka na urai wake na kufunguliwa kesi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Machi 17, mwaka huu.

“Awali alikamatwa kwa madai kuwa si raia lakini Mahakama Kuu ikadhibitisha kuwa ni raia halali lakini tangu wakati huo bado anashilikwa sasa sisi hatuelewi hadi sasa. Tunamuomba Rais wetu Dk.John Magufuli na serikali yake watusaidie suala hili,” alisema Mwaipungu

Kutokana na madai hayo mwandishi alimtafuta Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mmabosasa, ambapo alimtaka mwandishi wa habari hawe na subira wa suala hili kwani yupo nje ya ofisi.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles