27.2 C
Dar es Salaam
Wednesday, April 24, 2024

Contact us: [email protected]

EU WATISHIA KUIWEKEA VIKWAZO VENEZUELA

BEIJING, CHINA


UMOJA wa Ulaya (EU) umeonya utaiwekea vikwazo zaidi Venezuela na kutishia kuchukua hatua zaidi kama hizo iwapo demokrasia haitazingatiwa katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika kipindi cha mwezi mmoja kuanzia sasa.

Mkuu wa Sera za Nje wa EU, Federeca Moghereni, alisema katika taarifa yake kuwa amesikitishwa na uamuzi wa maofisa wa Venezuela chini ya Rais Nicolas Maduro.

Alisema haikuwa busara kwa maofisa hao kuamua kuitisha uchaguzi wa rais na Bunge Mei 20 bila kupatikana mwafaka juu ya taratibu zinazokubalika kuhusu mchakato huo.

Aliongeza kuwa Umoja wa Ulaya utafuatilia kwa karibu mchakato wa uchaguzi na kuwa uko tayari kuchukua hatua dhidi ya uamuzi au vitendo vyovyote vinavyolenga kuikandamiza demokrasia na utawala wa sheria nchini Venezuela.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles