23.9 C
Dar es Salaam
Wednesday, April 24, 2024

Contact us: [email protected]

Ernest Napoleon: Hatuwezi kuzuia uharamia wa kazi za wasanii

Ernest Napoleon Going BongoNA FESTO POLEA

MSHINDI wa tuzo ya East Afrika kupitia filamu yake ya ‘Going Bongo’, Ernest Napoleon, ameweka wazi kwamba haiwezekani kuzuia uharamia wa kazi za wasanii kwa kuwa hatuna sheria ya kufanya hivyo.

Napoleon alisema kuzuia uharamia wa kazi za wasanii kwa Tanzania itaendelea kuleta vilio kwa wasanii wake hadi mifumo itakaporekebishwa na sheria zikatungwa.

“Huo ndio ukweli wala tusidanganyane, hatuwezi kuzuia uharamia wa kazi za wasanii kwa kuwa hakuna sheria za kuzuia uharamia huo hivyo kila mtu anayeingiza fedha kwa wizi huo ataendelea kunufaika hadi sheria zitakapopatikana na mifumo ikabadilika,” alieleza Napoleon.

Napoleon ambaye anatarajia kuandaa filamu yake mpya atakayoichezea visiwani Zanzibar, aliongeza kwa kuwataka wasanii kuendelea kufanya kazi nzuri na kuhangaika kuzisambaza katika matamasha mbalimbali ili kujitangaza kwa ajili ya kutengeneza soko kubwa la filamu zao zijazo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles