LAS VEGAS, MAREKANI
UHUSIANO wao wa kimapenzi ulivunjika mwaka jana, lakini bado jina la mrembo Rihanna limeonekana kubaki kichwani kwa Drake mpaka leo hii.
Ripoti zimedai kwamba, Drake amekuwa akimtumia meseji Rihanna tangu zilipoibuka taarifa za mwanadada huyo kutoka na bilionea wa Saudi Arabia, Hassan Jameel. “Drake ‘anammis’,” kilisema chanzo kimoja kuuambia mtandao wa TMZ, ambao ni maarufu kwa habari za uhakika za wasanii.
Chanzo hicho kiliongeza kuwa, tayari Rihanna ameshajua kwamba Drake anamuonea wivu.
Mwezi uliopita, japo hazikuthibitishwa, kulikuwa na taarifa zilizodai Drake amekuwa akimshawishi Rihanna kutemana na tajiri Jameel, ili wafufue mapenzi yao.