23.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Dk Tulia aongoza mazishi ya Ndasa

Ramadhan Hassan -Dodoma

NAIBU Spika Dk. Tulia Akson ameongoza mazishi ya aliyekuwa Mbunge wa Sumve Richard Ndassa (61), ambaye alizikwa jana Sumve mkoani Mwanza.

Marehemu Ndassa alifariki juzi jijini Dodoma ambapo Spika wa Bunge Job Ndugai juzi alisema ni lazima mbunge huyo azikwe nyumbani kwake Sumve.

Jana mara baada ya kuanza na dua ya kuliombea Bunge na taifa kusomwa ikiwa ni kabla ya bajeti ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kuwasilishwa bungeni, Spika wa Bunge Ndugai, alisimamana kusema   Naibu Spika Dk. Tulia ndiye ambaye ataongoza mazishi ya Ndasa akiwa pamoja na  Mbunge wa Sengerema, William Ngeleja (CCM).

“Niwataarifu  mwili wa Richard Ndassa ndio umewasili pale Sumve muda huu (jana saa nane na robo) kwahiyo jioni hii mazishi yatafanyika waliondoka (Dodoma) saa 6 usiku  wa kuamkia leo (jana) tumewakilishwa na Ngeleja na Naibu Spika tunawatakia kila heri katika jambo hilo wanalotuwakilisha,” alisema Ndugai.

Ndassa anakuwa mbunge wa nane kufariki kwa kipindi cha miaka mitano tangu kuanza kwa bunge la 11.

Wengine waliofariki ni Mbunge wa Newala Vijijini (CCM), Rashid Akbar, Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Dk. Getrude Rwakatare, Mbunge wa Korogwe Vijijini (CCM), Stephen Ngonyani maarufu kama Profesa Majimarefu, Mbunge wa Viti Maalum (Chadema), Dk. Elly Macha, Mbunge wa Dimani (CCM), Hafidh Ally Tahir, Mbunge wa Songea Mjini (CCM), Leonidas Gama na  Mbunge wa Buyungu, Kasuku Bilago (Chadema).

Juzi Ndugai akitangaza kifo hicho, alisema “kwa masikitiko makubwa naomba kuwajulisha bunge letu limepatwa na msiba mwingine mkubwa wa kuondokewa na Mbunge mwenzetu Mbunge wa Sumve Richard Ndassa mbaye amefariki usiku wa kuamkia leo hapa Jijini Dodoma.

 “Kufuatia msiba huo tulioupata taratibu mbalimbaliza za mazishi zimeanza kufanyika kwa mawasiliano ya upande wa Serikali na familia. Na kila tukipata taarifa tutafanya hivyo,”alisema.

Atazikwa kijijini kwake

Ndugai alisema ofisi yake itahakikisha mbunge huyo leo jioni (jana) anazikwa katika kijiji chake huko, Sumve.

“Tutajitahidi sana iwezekanavyo kuhakikisha kwamba mheshimiwa huyu, ndugu yetu anazikwa kule Sumve kesho (jana) jioni ‘unless’ tumekuwa advice  otherwise (tumeshauriwa vinginevyo) kwa sababu kwa mila zetu za kiafrika kweli kumzika mtu  popote linatupa shida.

“Fikiria yeyote ambaye upo hapa unapatwa na jambo kama hilo halafu unawekwa popote, kwahiyo tutajitajidi sana ofisi yangu itashirikiana na Seriklai kuona kila kinachowezekana kinafanyika,”alisema.

Akizungumzia Ndassa, Spika alisema aliingia bungeni mwaka 1995 ambapo na kwamba amelitumikia Bunge kwa kipindi cha miaka 25 kwa vipindi vitano tofauti.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles