27 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Di Maria kuikosa michezo iliyobaki Copa America

 Di Maria
Angel Di Maria

NEW YORK, MAREKANI

NYOTA wa timu ya Taifa ya Argentina, Di Maria atakuwa nje ya uwanja katika michuano ya Copa America Centenario, kutokana na kusumbuliwa na nyama za paja.

Mchezaji huyo alipata matatizo hayo katika mchezo wa mwishoni mwa wiki iliyopita wakati timu yake ikiibuka na ushindi wa mabao 5-0 dhidi ya Panama, katika kipindi cha pili cha mchezo huo na nafasi yake ikachukuliwa na Erik Lamela.

Madaktari wamedai kwamba, mchezaji huyo anaweza kuwa nje ya uwanja kwa muda wa wiki tatu, hivyo michuano hiyo itakuwa ipo katika hatua za mwisho kumalizika.

Lakini anaweza kucheza katika mchezo wa fainali kama timu yake ya Argentina itafanikiwa kufika hatua hiyo.

Mchezaji huyo alijaribu kufanya mazoezi juzi lakini alishindwa kutokana na maumivu na kujikuta akidondosha chozi huku ikidaiwa kwamba anaililia timu yake ambapo alipanga kuisaidia katika michuano hii.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles