29.2 C
Dar es Salaam
Wednesday, April 24, 2024

Contact us: [email protected]

DC KITETO ATAKA WAFUGAJI KUCHANGIA ELIMU

Mohamed Hamad, Manyara

Mkuu wa Wilaya ya Kiteto mkoani Manyara, Tumaini Magesa amewataka wananchi wa Kijiji cha Ilkiushbor kuuza mifugo yao na kujenga mabweni ili watoto wao waondokane na adha ya kutembea umbali mrefu kwenda shuleni.

Akizungumza na wananchi wa Kijiji hicho Magesa amesema watoto wengi wilayani humo hawaendi shule kutokana na umbali ambapo hutumia muda mwingi njiani wakielekea shuleni.

“Hali hiyo imesababisha utoro ambapo wengi wao huacha shule pamoja na wengine hupata mimba za utotoni,” amesema.

Kutokana na hali hiyo, Magesa amesema jitihada za Serikali ni kuhamasisha wananchi kujenga mabweni hadi kufikia hatua ya kuezeka kisha wao watamalizia.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles